Pages

Friday, 24 October 2014

USUMBUFU WA WAPIGADEBE UBUNGO BADO NI KERO.



Ni muda mrefu umepita baada ya mamlaka yainayoshughulika na usafiri wan chi kavu na majini SUMATRA, walipotoa amri ya kupiga marufuku wapigadebe wa kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungo,wasiokua na sare kuwasumbua abiria.



                



Kwa kipindi kifupi tu tatizo hilo lilikomeshwa kwa kutumia nguvu za ziada na hatimae wakawaondoa wapigadebe wote waliokuwawanafanya kazi kiholela  na hatimae usumbufu ulipungua.

Kutokana na kutokuwepo kwa mipango endelevu hali ile ya mwanzo imejirudia tena, ila sasa inatisha kwani wapigadebe wamekuwa wengi mno kiasi kwamba hata wale wenye sare hawaonekani.




                 



Kitu cha ajabu zaidi wapigadebe wasiovaa sare ndio wamekuwa kipaombele kwa kuwapokea wabiria na kuwapeleka ofisi za mabasi husika kwa nia ya kukata tikiti. Hali hii imepelekea kwa wale abiria wageni wa jiji la Dar es salaam, kulizwa kila kukicha  ambapo  wamekuwa wakitapeliwa mizigo yao  pamoja na vitu vingine vidogo vidogo kama nauli na simu za mikononi.
 

Kwa kuwa mpango huu ulianza kwa malengo dhabiti Sumatra hawanabudi kujipanga tena upya kwaajili ya kuikomesha kero hii ambayo imekuwa ikitoa picha chafu kwa wageni wanaofika jijini Dar es salaa.


No comments:

Post a Comment