Pages

Tuesday, 30 September 2014

HILI NALO LINAHITAJI ELIMU?

Licha yakuwa na sifa kedekede Jiji la Dar es salaam limeendelea kuwa chafu kila kukicha kutokana na baadhi ya wakazi kutojua umuhimu wa kutunza mazingira.







kutokana na kutokujua kwao kumepelekea karibu kila kona  ya jiji hili kuwa na harufu mbaya iliyotapakaa kila mahali.

Baadhi ya wakazi hasa waishio maeneo ya uswahilini wamegeuza vituo vya Daladala kuwa kama sehemu maalumu za kuweka uchafu, cha kushangaza ni kuwa mara kadhaa wamekuwa wakitupa mchana kweupe bila ya kuchukuliwa hatua yoyote.

 Ni bora taka hizo zingekuwa zakawaida lakini cha ajabu wengine wanathubutu kutupa kinyesi pamoja na mikojo iliyowekwa kwenye chupa za maji safi.



    






                               

                                                                

Wengine wamejiwekea ratiba ya kutupa taka zao sehemu zisizo rasmi, mara nyingi utawaona muda wa usiku na mapema asubuhi wakiwa wamebeba mafurushi makubwa utafikiri wasafiri, kumbe wanatafuta sehemu za kutupa taka zao.

Kutokana na kutapakaa kwa taka hizo kumepelekea milipuko ya magonjwa mbalimbali hasa kipindi cha mvua magonjwa kama kipindupindu, kichocho na taifodi yamekuwa yakiwaadhili hasa watoto wadogo.  

Monday, 29 September 2014

MAEGESHO YA MAAGARI NI TATIZO MJINI.



Kutokana na kutokuwepo kwa mpangilio mzuri wa maegesho ya magari (PARKING) pamoja na pikipiki jijini Dar es Salaam, kumepelekea tishio kubwa kwa watembea kwa miguu kukumbana na ajali katika nyakati tofauti.



Moja ya sehemu za kuegeshea magari katika mitaa ya kariakoo
                                              


 Kuanzia mazingira pamoja na ufinyu wa maegesho hayo ambayo siyo rafiki kabisa na wakazi wa jiji hili, ambao mara zote wamekuwa na pilikapilika za hapa na pale kwaajili ya kujiingizia kipato chao cha kila siku.

kuna maswali mengi yakujiuliza juu ya wahusika hasa serikali ambayo imekuwa muhusika katika mpangilio wa makazi ya watu pamoja na miundo mbinu kama ya Barabara, mosi kama walijua wafanyakazi wa mjini karibia wote wanamiliki vyombo vya usafiri, kwanini hawakuandaa sehemu maalumu za kuegeshea magari yao? Pili sheria za mipango
miji na zile za barabarani zinaruhusu uegeshaji wa magari kwa vipimo vipi?

Binafsi makazi yoyote yale inabidi yawe umbali wa mita 100, ambayo ndiyo hifadhi ya barabara. Je kwa ukaribu ule wa maegesho ya mitaa ya kariakoo na sehemu nyingine hapa mjini ni mita 100?

Friday, 26 September 2014

YOUNG DEE, APATA SHAVU JIPYA.




Msanii Young Dee a.k.a paka rapper ambaye anafanya vizuri katika muziki wa rap mpaka sasa, ameingia mkataba mnono na kampuni ya Star Times inayojishughulisha na uuzaji wa ving'amuzi kuwa balozi wa channel ya Qyou hapa nchini.

Young Dee ambaye hivi karibuni aliachia wimbo wake mpya unaoitwa "SIO MCHOYO" aliomshirikisha mkali wa R&B bongo Jux a.k.a V tone amekaririwa na Bongo5 kuwa, Star Times wamemlipa kile alicho staili na ndio maana amekubali kusaini mkataba huo.



Young Dee kwa nyuma akiwa ameshika makata



"Nimesaini mkataba na Star Times kutumia picha yangu na pia kama balozi wa Qyou channel ya vijana, kuhusu kunilipa ni jambo langu binafsi ila jua inanilipa vizuri  ndio maana nimekubali kufanya kazi hiyo". Amesema Young Dee.

Thursday, 25 September 2014

MASHABIKI WAMSUBIRI KWA HAMU SUAREZ.

Mshambuliaji machachari anayekipiga katika miamba wa hispania Barcelona FC, Luis Suarez anasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa timu ya Barcelona wakimuona akitandaza kabumbu dimbani hivi karibuni. habari zaidi click HAPA.
LUIS SUAREZ.

Wednesday, 24 September 2014

YOUNG KILLER "NINAFURAHA KUSHIRIKISHWA NA MKONGWE."

kijana mdogo anayefanya vizuri kwa sasa nchini tanzania katika muziki wa hip hop Young killer a.k.a msodoki the son, amesema ana furaha sana baada ya  kushirikishwa na mkongwe aliyekulia katika familia ya muziki banana zoro.
Young killer, Zahir na Banana
katikati ya mwaka huu young killer aliachia wimbo wake mpya "umebadilika" alio mshirikisha mkongwe huyo hivyo basi kutokana na kupokelewa vizuri kwa wimbo huo Banana aliamua kumshirikisha katika wimbo wake huo mpya "samehe sahau" uliotengenezwa katika studio za Dully Syles, 4,12. kwa undani zaidi click HAPA.

Tuesday, 23 September 2014

MIGOGORO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI INAHITAJI SULUHISHO LA KUDUMU.


Askari wa jeshi la kutuliza gasia wakikabiliana na wakulima

Umepita muda sasa mgogoro kati ya wakulima na wafugaji katika kijiji cha laitimi mkoani Dodoma bado hauja tafutiwa ufumbuzi huku baadhi ya wakulima na wafugaji wakiripotiwa kuuwawa.

Kila jamii imekuwa ikidai kuwa wao ndio wamiliki halali wa eneo hilo ambalo limekuwa likiwaingiza katika mgogoro mkubwa kila mwaka hasa ifikapo kipindi cha masika na kiangazi, ambapo kwa muda huo wakulima wanakuwa katika uzalishaji na mavuno huku wafugaji wakitafuta maeneo ya malisho kwaajili ya mifugo yao.

Kutokana na sintofahamu hiyo kuhusu ni nani mmiliki halali wa eneo hilo kati ya wakulima ambao ni jamii ya wagogo na wabena dhidi ya wafugaji jamii ya wamasai wengi wao wakitokea mikoa ya kaskazini yaani manyara na kiteto, hivyo basi kila jamii inajiona inamamlaka zaidi kuliko mwenzake.

Kwakuwa mgogoro huu bado haujapata utatuzi wa kudumu machafuko yamekuwa yakiendelea kila kukicha huku jamii kubwa inayo adhilika ni wakulima hasa kabila la wagogo, vifo hivyo vimekuwa vikitokea hasa kwa kabila la wagogo kwasababu mara nyingi wamekuwa vibarua walioajiliwa na watu wa jamii ya wabena hivyo katika kipindi chote cha kilimo huishi katika mashamba.

Jitihada kubwa Zimekuwa Zikifanywa na vingozi mbalimbali wakijaribu kutatua mgogoro huu akiwemo mbunge wa Dodoma mh. Jobu ndugai, japokuwa jitihada zake bado hazijaonesha mafanikio yoyote hadi sasa.


Mgogoro huu sio wa Ndugai peke yake au wakulima na wafugaji wa mkoa wa Dodoma tu, yatupasa jamii yote ya watanzania kushirikiana kwanguvu ili kushuluhisha mgogoro huu kama si kuumaliza kabisa kwakuwa hakuna kisicho wezekana endapo tutawekania dhabiti katika jamobo hili. 

Wakulima wakichangia jambo ka


Monday, 22 September 2014

KERO HII MPAKA LINI?



Kumekuwa na tatizo ambalo limekuwa likiwatesa abiria waendao mbezi kutoka kariakoo la kupigana vikumbo na wapiga debe wa kituo cha daladala cha karikoo madukani.


Pindi ifikapo muda wa mchana na jioni wananchi wamekuwa wakisumbuliwa na wapiga debe ambao wamekuwa na tabia ya kugombea siti za daladala kwa nia ya kuwalipisha abiria ndipo wapate kukaa kama sio hivyo watasimama.

jambo hili lilianza kitambo sana ila kwa sasa imekuwa kama ajira kwa wapiga debe wa kariakoo imefika wakati kila daladala inapofika hukimbilia kwa kasi utadhani wao ni wasafiri, na pia wamekuwa wakiwaibia baadhi ya abiria vitu mbalimbali ikiwemo mikoba, pesa, na simu za mkononi.

Kwa ujumla maisha ya wakazi wa mbezi yamekuwa magumu kwao kwani wamekuwa wakilipa nauli mara mbili zaidi ya ile iliyopangwa na SUMATRA. 


Baadhi ya makondokta wamekua chanzo kikuu cha kuwatoza abiria kiwango kikubwa cha pesa na tatizo hilo limepelekewa na kukatizwa kwa safari ilikupata  faida zaidi kwa manufaa yao binafsi.

Wapiga debe wamekuwa wakiwahia viti vya daladala kwaajili ya kupata ujira wa shilingi 500 mpaka 1000 na huwa wakali kama mbogo endapo wakikuachia nafasi ya kukaa halafu usiwape haki yao.

Kuna umuhimu mkubwa sana wa jamii na watu husika kulitambua jambo hili kama kero kubwa, lakini ni jambo la msingi kutatua hili tatizo kwa nia ya kuzuia baadhi ya matatizo kama ya kuibiwa pamoja na kupunguza gharama za maisha.   



kituo cha daladala kariakoo madukani.