Pages

Monday, 29 September 2014

MAEGESHO YA MAAGARI NI TATIZO MJINI.



Kutokana na kutokuwepo kwa mpangilio mzuri wa maegesho ya magari (PARKING) pamoja na pikipiki jijini Dar es Salaam, kumepelekea tishio kubwa kwa watembea kwa miguu kukumbana na ajali katika nyakati tofauti.



Moja ya sehemu za kuegeshea magari katika mitaa ya kariakoo
                                              


 Kuanzia mazingira pamoja na ufinyu wa maegesho hayo ambayo siyo rafiki kabisa na wakazi wa jiji hili, ambao mara zote wamekuwa na pilikapilika za hapa na pale kwaajili ya kujiingizia kipato chao cha kila siku.

kuna maswali mengi yakujiuliza juu ya wahusika hasa serikali ambayo imekuwa muhusika katika mpangilio wa makazi ya watu pamoja na miundo mbinu kama ya Barabara, mosi kama walijua wafanyakazi wa mjini karibia wote wanamiliki vyombo vya usafiri, kwanini hawakuandaa sehemu maalumu za kuegeshea magari yao? Pili sheria za mipango
miji na zile za barabarani zinaruhusu uegeshaji wa magari kwa vipimo vipi?

Binafsi makazi yoyote yale inabidi yawe umbali wa mita 100, ambayo ndiyo hifadhi ya barabara. Je kwa ukaribu ule wa maegesho ya mitaa ya kariakoo na sehemu nyingine hapa mjini ni mita 100?

No comments:

Post a Comment