Msanii Young Dee a.k.a paka rapper ambaye anafanya vizuri katika muziki wa rap mpaka sasa, ameingia mkataba mnono na kampuni ya Star Times inayojishughulisha na uuzaji wa ving'amuzi kuwa balozi wa channel ya Qyou hapa nchini.
Young Dee ambaye hivi karibuni aliachia wimbo wake mpya unaoitwa "SIO MCHOYO" aliomshirikisha mkali wa R&B bongo Jux a.k.a V tone amekaririwa na Bongo5 kuwa, Star Times wamemlipa kile alicho staili na ndio maana amekubali kusaini mkataba huo.
"Nimesaini mkataba na Star Times kutumia picha yangu na pia kama balozi wa Qyou channel ya vijana, kuhusu kunilipa ni jambo langu binafsi ila jua inanilipa vizuri ndio maana nimekubali kufanya kazi hiyo". Amesema Young Dee.

No comments:
Post a Comment