Pages

Wednesday, 1 October 2014

MADEREVA BODABODA WAPEWE ELIMU YA USALAMA.

Madereva wa pikipiki (Bodaboda) jijini Dar es salaam wanatajwa kuwa chanzo kikuu cha ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara na kupelekea vifo au ulemavu kwa uzembe uliopitiliza.









Asilimia kubwa ya madereva hao wamekua wakiendesha pikipiki kwa mwendo kasi mno bila ya kujali usalama wao wala watembea kwa miguu.

Sheria zimekuwa zikifunjwa tena kwa makusudi kiasi kwamba madereva hao, hawakupitia shule ijapokuwa sheria pamoja na askari wa usalama barabarani kuweka mkazo katika utekelezwaji huo wa sheria, kama vile kuvaa kofia ngumu kichwani ambapo madereva wengi wamekuwa hawatii amri matokeo yake hupoteza maisha mara tu baada ya kupata ajali.







Lakini sio jambo la ajabu kwa madereva kuvunja sheria hizo, kwa kuwa kunabaadhi ya madereva wameletewa leseni za udereva majumbani mwao huku wengine hawana kabisa vigezo na hata hizo leseni hawajui zipo katika muundo gani.

Huu ni ushauri wa bure kwa maderea na wanajamii kwa ujumla yatupasa kutambua kuwa mabadiliko yanaanzia kwako.



No comments:

Post a Comment