Pages

Monday, 6 October 2014

HATUNA BUDI KUWAJIBIKA KATIKA HILI.



Wakati umefika sasa kwa polisi wa usalama barabarani Jijini Dar es salaam wakishirikiana na wadau wengine kukemea kwa nguvu kero ya vyombo vya moto hasa pikipiki na magari ambapo madereva wake wamekuwa wakilazimisha kupita sehemu maalumu ambazo zimetengenezwa kwaajili ya watembea kwa miguu. 








 Jambo hili limekuwa likitishia uhai wa watembea kwa miguu jijini Dar es salaam ambao mara nyingi wamekuwa wakipata misukosuko ya hapa na pale ya  kunusulika kugongwa na magari na pikipiki hasa inapofika majira ya jioni ambapo wengi huwa wamejikita hasa katika matumizi ya  simu zao za mkononi huku wengine wakiwa na pilikapilika za kuwahi usafiri.

Hatuna budi kuwajuza madereva wote ambao wamekuwa na haraka ya kufika makwao zaidi yaw engine yakuwa zile barabara zimetengenezwa kwaajili ya watembea kwa miguu tu, kwahiyo ni lazima waheshimu sheria na taratibu za barabarani.

Nina imani ya kuwa serikali iliona ipo haja ya kuwatengenezea wananchi wake semu zao maalumu za kutembelea. Sasa ni kivipi madereva wale wasiojiheshimu  wanadhubutu kupuuza agizo ilo la serikali?









Hakika mazoea haya sio mazuri hata kidogo kwa sababu tabia hii itaota mizizi ambayo itakomaa huku wananchi wakiendelea kukumbwa na vifo pamoja na ulemavu unaosababishwa na baadhi ya  madereva  wazembe.

Hili sio suala la polisi wa usalama pekee bali ni la watu wote wapenda maendeleo na mabadiliko, lakini ni muhimu kwa vyombo vya dola kuweka sheria madhubuti zitakazoweza kuwabana madereva wanaovunja sheria na kukabiliana nazo kwa wakati sahihi.




No comments:

Post a Comment