Pages

Tuesday, 23 September 2014

MIGOGORO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI INAHITAJI SULUHISHO LA KUDUMU.


Askari wa jeshi la kutuliza gasia wakikabiliana na wakulima

Umepita muda sasa mgogoro kati ya wakulima na wafugaji katika kijiji cha laitimi mkoani Dodoma bado hauja tafutiwa ufumbuzi huku baadhi ya wakulima na wafugaji wakiripotiwa kuuwawa.

Kila jamii imekuwa ikidai kuwa wao ndio wamiliki halali wa eneo hilo ambalo limekuwa likiwaingiza katika mgogoro mkubwa kila mwaka hasa ifikapo kipindi cha masika na kiangazi, ambapo kwa muda huo wakulima wanakuwa katika uzalishaji na mavuno huku wafugaji wakitafuta maeneo ya malisho kwaajili ya mifugo yao.

Kutokana na sintofahamu hiyo kuhusu ni nani mmiliki halali wa eneo hilo kati ya wakulima ambao ni jamii ya wagogo na wabena dhidi ya wafugaji jamii ya wamasai wengi wao wakitokea mikoa ya kaskazini yaani manyara na kiteto, hivyo basi kila jamii inajiona inamamlaka zaidi kuliko mwenzake.

Kwakuwa mgogoro huu bado haujapata utatuzi wa kudumu machafuko yamekuwa yakiendelea kila kukicha huku jamii kubwa inayo adhilika ni wakulima hasa kabila la wagogo, vifo hivyo vimekuwa vikitokea hasa kwa kabila la wagogo kwasababu mara nyingi wamekuwa vibarua walioajiliwa na watu wa jamii ya wabena hivyo katika kipindi chote cha kilimo huishi katika mashamba.

Jitihada kubwa Zimekuwa Zikifanywa na vingozi mbalimbali wakijaribu kutatua mgogoro huu akiwemo mbunge wa Dodoma mh. Jobu ndugai, japokuwa jitihada zake bado hazijaonesha mafanikio yoyote hadi sasa.


Mgogoro huu sio wa Ndugai peke yake au wakulima na wafugaji wa mkoa wa Dodoma tu, yatupasa jamii yote ya watanzania kushirikiana kwanguvu ili kushuluhisha mgogoro huu kama si kuumaliza kabisa kwakuwa hakuna kisicho wezekana endapo tutawekania dhabiti katika jamobo hili. 

Wakulima wakichangia jambo ka


No comments:

Post a Comment