Pages

Tuesday, 21 October 2014

SERIKARI IMESHINDWA KUZUIA ONGEZEKO LA GEREJI BUBU?


Kumekuwa na malalamiko mengi ambayo yamekuwa yakitolewa na wakazi wa jiji la Dar es salaam, juu ya wingi wa sehemu za kutengenezea vyombo yva usafiri maarufu kama Gereji bubu           kuwepo kwa kila mtaa.









Hali hiyo imesababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wanao ishi kando kando mwa gereji hizo, ambao wamekuwa wakikerwa hasa na kelele zinazotokana na mashine wanazozitumia mafundi wakati wa ukataji wa vyuma pamoja na kauli chafu za baadhi ya mafundi.

Kutokana na kuongezeka kwa gereji hizo zisizo rasmi kunatishia usalama wa raia waishio karibu na maeneo hayo, kwa sababu inaweza kutokea mlipuko wowote utakao sababishwa na mafuta ya petrol au disel.

Ijapokuwa serikari imekuwa ikijitahidi katika hili na kuzifungia baadhi ya gereji bubu, lakini bado baadhi ya watu wameendelea kufungua kiholela bila ya kujali eneo pamoja na usalama wa wakazi wa karibu na maeneo husika.


No comments:

Post a Comment