Umefika wakati
wakujiuliza ni lini hasa malumbano na migogoro ya wafanyabiashara wadogowadogo
maarufu kwa jina la wamachinga na uongozi wa jiji la Dar es salaamambao
haujapatiwa ufumbuzi hadi leo.
Kila upande umekuwa
ukitoa sababu zake tena zakueleweka, lakini bado haujifikiwa muafaka mzuri juu
ya mgogoro huo. Kwa upande wa serikali wamekuwa wakijitetea kuwa
wameshawatengea maeneo maalumu ya kufanyia biashara mfano mzuri ni lile jengo
lililopo ilala la MACHINGA COMPLEX.
Kwa upande mwingine
wafanyabiashara wadogowadogo wamekuwa wakiilalamika kuwa serikali imekuwa
ikiwatoza kiwango kikubwa katika vitalu na pia maeneo waliyotengewa hayana
mvuto kwa wateja.
Kutokana na kutofikiwa
kwa muafaka wa mgogoro huo kumepelekea kutapakaa kwa wamachinga sehemu
mbalimbali ndani ja jiji la Dar es salaam kama Manzese, Kariakoo na Ubungo.
Serikali kwa
kushirkiana na wamachinga haina budi kukaa chini na kutafuta suluhisho la
mgogoro huu, kwa kuwa mgogoro huu sio wa Dar es salaam peke yake bali ni kero
karibia Tanzania nzima mikoa kama ya mwanza na mbeya migogoro hii imekuwa
ikiibuka kila wakati.
Kiasi kwamba wamachinga
wamekuwa wakivamia maeneo yasiyo rasmi na kusababisha ufinyu wa maeneo kama
vile barabara na vituo vikuu vya kapakia na kushushia abiria


No comments:
Post a Comment