Pages

Thursday, 9 October 2014

MALUMBANO SIO SULUHISHO SAHIHI LA MIGOGORO.



Umefika wakati wakujiuliza ni lini hasa malumbano na migogoro ya wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kwa jina la wamachinga na uongozi wa jiji la Dar es salaamambao haujapatiwa ufumbuzi hadi leo.








Kila upande umekuwa ukitoa sababu zake tena zakueleweka, lakini bado haujifikiwa muafaka mzuri juu ya mgogoro huo. Kwa upande wa serikali wamekuwa wakijitetea kuwa wameshawatengea maeneo maalumu ya kufanyia biashara mfano mzuri ni lile jengo lililopo ilala la MACHINGA COMPLEX.

Kwa upande mwingine wafanyabiashara wadogowadogo wamekuwa wakiilalamika kuwa serikali imekuwa ikiwatoza kiwango kikubwa katika vitalu na pia maeneo waliyotengewa hayana mvuto kwa wateja.

Kutokana na kutofikiwa kwa muafaka wa mgogoro huo kumepelekea kutapakaa kwa wamachinga sehemu mbalimbali ndani ja jiji la Dar es salaam kama Manzese, Kariakoo na Ubungo.






 
Serikali kwa kushirkiana na wamachinga haina budi kukaa chini na kutafuta suluhisho la mgogoro huu, kwa kuwa mgogoro huu sio wa Dar es salaam peke yake bali ni kero karibia Tanzania nzima mikoa kama ya mwanza na mbeya migogoro hii imekuwa ikiibuka kila wakati.
 
Kiasi kwamba wamachinga wamekuwa wakivamia maeneo yasiyo rasmi na kusababisha ufinyu wa maeneo kama vile barabara na vituo vikuu vya kapakia na kushushia abiria

No comments:

Post a Comment