Kumekuwa na tatizo
ambalo limekuwa likiwatesa abiria waendao mbezi kutoka kariakoo la kupigana
vikumbo na wapiga debe wa kituo cha daladala cha karikoo madukani.
Pindi ifikapo muda wa
mchana na jioni wananchi wamekuwa wakisumbuliwa na wapiga debe ambao wamekuwa
na tabia ya kugombea siti za daladala kwa nia ya kuwalipisha abiria ndipo wapate
kukaa kama sio hivyo watasimama.
jambo hili lilianza
kitambo sana ila kwa sasa imekuwa kama ajira kwa wapiga debe wa kariakoo
imefika wakati kila daladala inapofika hukimbilia kwa kasi utadhani wao ni
wasafiri, na pia wamekuwa wakiwaibia baadhi ya abiria vitu mbalimbali ikiwemo
mikoba, pesa, na simu za mkononi.
Kwa ujumla maisha ya
wakazi wa mbezi yamekuwa magumu kwao kwani wamekuwa wakilipa nauli mara mbili
zaidi ya ile iliyopangwa na SUMATRA.
Baadhi ya makondokta wamekua
chanzo kikuu cha kuwatoza abiria kiwango kikubwa cha pesa na tatizo hilo
limepelekewa na kukatizwa kwa safari ilikupata
faida zaidi kwa manufaa yao binafsi.
Wapiga debe wamekuwa
wakiwahia viti vya daladala kwaajili ya kupata ujira wa shilingi 500 mpaka 1000
na huwa wakali kama mbogo endapo wakikuachia nafasi ya kukaa halafu usiwape
haki yao.
Kuna umuhimu mkubwa
sana wa jamii na watu husika kulitambua jambo hili kama kero kubwa, lakini ni
jambo la msingi kutatua hili tatizo kwa nia ya kuzuia baadhi ya matatizo kama
ya kuibiwa pamoja na kupunguza gharama za maisha.
![]() |
| kituo cha daladala kariakoo madukani. |

No comments:
Post a Comment